-->

Kutoka Dar es salaam, Wasichana 500 wa shule za secondary na shule za msingi Kupewa Taulo Za kike Zinazotumika Na Kufuliwa


  1. New


    [​IMG]


    Dar es Salaam. Wasichana 500 wa shule mbalimbali za msingi na sekondari jijini Dar es Salaam, kesho watanufaika na taulo za kike zinazoweza kufuliwa na kutumika tena.

    Ugawaji wa pedi hizo unafanyika katika maadhimisho ya siku ya hedhi duniani kesho.

    Maadhimisho hayo yatakayofanyika katika bwalo la maofisa wa polisi, yanafanyika wakati asilimia 65 ya wanawake na wasichana nchini Tanzania wakishindwa kumudu kutumia pedi katika siku zao za hedhi.

    Akizungumza na vyombo vya habari leo Mei 27, Mkurugenzi wa Asasi ya Chief Promotions, Amon Mkoga amesema zaidi ya wasichana 850,000 wanakosa wiki sita za masomo kila mwaka huku wanawake wakipoteza saa zao za kufanya kazi.



    “Kesho tutagawa pedi kwa watoto zaidi ya 500 wa shule mbalimbali za msingi na sekondari, tutakuwa na pedi aina mbili ambazo ni zile za kutumia na kufua ‘relief pad’ anaweza akavaa mwaka mzima pamoja na HQ,” amesema Mkoga.

    Amesema katika matembezi hayo ya hisani, yatakayoongozwa na Naibu Waziri wa Afya Dk Faustine Ndugulile kutakuwa na wasambazaji wa pedi ambao watakuwa na mabanda yao.

    “Tatizo ni kubwa kwa eneo lolote lenye umaskini tutazungumza nini kinafanyika mwaka huu lakini pia kuna wadau maalum ambao wanawaangalia watu mbalimbali wenye mahitaji maalum wanapatiwa msaada kwa mwaka mzima hawa tutawatambua kupitia viongozi wao wa kata,” amesema.

    Meneja wa kampuni ya Relief Pad inayozalisha pedi za kudumu, Sangamesh Salimaly amesema pedi hizo za kutumia na kufua zimetengenezwa kwa malighafi maalum ambazo zinaweza kuhifadhi pasipo kuvujisha na kumfanya mhusika awe mkavu muda wote.

    “Ndani ya pikiti moja zinakaa pedi tano, moja ni kubwa, hizi mhusika anatumia na kufua na zinaweza kukaa kwa muda wa mwaka mzima bila kuharibika,” amesema Salimaly.

    MCL

Read also-: