-->

CWT yaunga mkono juhudi zinazofanywa na Makamu wa rais Samia Suluhu.



Katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa na makamu wa rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan za kuhamasisha suala la kufanya mazoezi kwa lengo la kuboresha afya za watanzania chama cha walimu Tanzania (CWT) kimekabidhi vifaa vya michezo kwa shule 15 za msingi na sekondari zilizo katika halmashauri ya wilaya ya bukoba iliyoko mkoani Kagera.
Vifaa vilivyokabidhiwa ni mipira ambayo itatumiwa na walimu pamoja na wanafunzi kwa ajili ya kufanya mazoezi ya mchezo wa mpira wa miguu, mpira wa pete, mpira wa wavu na mpira wa mikono, vifaa hivyo vimekabidhiwa leo na mwenyekiti wa chama cha walimu wa wilaya ya Bukoba, Methodius Majojo wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja vya ofisi ya chama hicho ambaye ameahidi kuwa zoezi la kugawa vifaa vya michezo kwamba litakuwa endelevu.
Kwa upande wao baadhi ya walimu wa shule 15 zilizopata vifaa hivyo kwa nyakati tofauti wamepongeza uamzi wa CWT wa kuunga juhudi za makamu wa Rais za kuhamasisha suala la mazoezi hivyo wakaziomba taasisi nyingine ziige mfano wa chama hicho huku wakionyesha imani yao kuwa kupitia michezo wanafunzi watajengeka kitaaluma zaidi.

Read also-: