-->

WAKALA VYUO VIKUU VYA NJE AIOMBA SERIKALI KUANGALIA MFUMO HATI YA KUSAFIRIA KWA WANAFUNZI

Na Ripota Wetu,Globu ya jamiiMKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni ya Wakala  ya Vyuo Vikuu vya Nje ya Darwin, Joseph Makungu amesema mfumo mpya wa hati ya kusafiria unapaswa kuwangalia wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vikuu vya nje ambao hawana sifa ya kupata hati hiyo kutokana kutofikisha miaka 18 ya kuweza kupata hati hizo.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi huyo amesema mamlaka zinazotoa vitambulisho ni vema kuangalia kundi hilo ili kupata hati ya kusafiria pale wanapohitaji kwa ajili ya masomo katika vyuo vikuu vya nje.
Amesema hati ya kusafiria ambayo imeanza kutolewa ni ya viwango vya kimataifa ambapo Tanzania imeweza kuthubu katika kwenda na wakati.
Makungu amesema wakala wa vyuo vikuu vya nje  kutokana na mfumo wa hati ya kusafiria kwa idara ya uhamiaji kuweza kuwapa elimu juu ya mfumo wakaulewa ili mbele ya safari wasipate usumbufu kwa wanafunzi pale wanapotaka kusafiri kwa masomo katika vyuo vikuu vya nje.Mkurugenzi Mtendaji Kampuni ya Uwakala wa Vyuo Vikuu vya Nje, Joseph Makungu akizungumza na waandishi habari kuhusiana na mfumo wa Hati ya Kusafiria, jijini Dar es Salaam.

Read also-: