-->

Zaidi ya wanafunzi elfu 30 wakosa udahili elimu ya juu mwaka huu

SeeBait
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako
Zaidi ya wanafunzi elfu thelathini walioomba kujiunga na masomo ya elimu ya juu nchini wamekosa udahili baada ya kushindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa na mwisho wa udahili ni hii leo saa sita usiku
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema hayo katika mahojiano maalumu TBC ambapo amevionya vyuo vilivyofungiwa udahili kutodahili wanafunzi.
Kuhusu utayari mazingira wezeshi kwa wanafunzi wenye ulemavu katika shule mbalimbali, serikali imekiri bado mazingira siyo wezeshi hususani katika shule za msingi.

Read also-: